Kuna mambo mengi au hali flani inaweza kuwa inajitokeza kwako mara kwa mara na usijue ni nini, au ukapuuzia lakini baadae ikaja kukuletea madhara makubwa. Ukiona mtu au kuhisi dalili zifuatazo, ujue ndio mwanzo wa stress Kimbia ukapate msaada kabla mambo hayajaharibika 1. Kutojiamini
2. Kujawa na mawazo mengi kichwani (Msongo wa mawazo)3. Kuwazia mabaya wakati wote
4. Kuongea kwa sauti (Shouting)
5. Kula chakula au kunywa pombe kupindukia
6. Kushindwa kula (Kupoteza hamu ya chakula)
7. Kushindwa kujichanganya na watu (Anti-Social)
8. Kusahau vitu mara kwa mara 9. Kupata tabu ku concentrate katika mambo
10.Matatizo ya tumbo, mdomo kukauka, misuli kukaza na kutoka jasho mara kwa mara
11. Kuamka mapema
12. Moyo kwenda mbio
13. Kusikia joto
14. Kichwa kuuma
YAFANYIE KAZI KABLA HUJACHELEWA
11 comments:
da lady hongera sana kwa somo zuri but nini dawa yake
Ooh Mungu nna hiyo kitu inansumbua kweli. So dawa yake nini?
jamani mbona mimi nina dalili karibu zote tib please..ila sinywi pombe na sina hamu ya kula
(1) Kuumwa Kichwa kila siku (2) Kukosa usingizi na kuamka mapema sana au kulala mapema sana na kuamka umechoka sana(3) Kukauka midomo (4) Kupayuka au kuwa na temper kitu kidogo nacharuka km pilipili imewekwa kwenye kidonda, na kuwa mkali kupita kiasi (5)sometimes kukosa hamu yakula sometimes kula sana (6)Kutojichanganya na watu (7) kutokujiamini haya yote ninayo kwahiyo mimi nastress ngapi? naenda hospital au kumuona mwanasaikolojia km aunt sadaka au? nisaidie pls
jamani dawa hakuna dawa kama dawa ila haya ni tiba tosha ya stress kubwa ni kujichangaya na watu, tafuta mtu wa kuongea nae unaemuamni lakin, fanya kitu ukipendacho unapokuwa stressed kama ni kusikiliza music, kuimba, kupiga au kufua kucheza sio kulala wa pombe, epuka kukaa mazingira hayo hayo kwa muda mrefu, pia pumzika kama vile beach, bustanini, au sehemu yoyte ile ambayo utafurahi ila sio yenye kelele zisizo na mpangilio kama vile sokoni au bar kwani stress ndo zitazidi. ni hayo tu wadau
jamani dawa hakuna dawa kama dawa ila haya ni tiba tosha ya stress kubwa ni kujichangaya na watu, tafuta mtu wa kuongea nae unaemuamni lakin, fanya kitu ukipendacho unapokuwa stressed kama ni kusikiliza music, kuimba, kupiga au kufua kucheza sio kulala wa pombe, epuka kukaa mazingira hayo hayo kwa muda mrefu, pia pumzika kama vile beach, bustanini, au sehemu yoyte ile ambayo utafurahi ila sio yenye kelele zisizo na mpangilio kama vile sokoni au bar kwani stress ndo zitazidi. ni hayo tu wadau
Dalili ya 7 KUSHINDWA KIJICHANGANYA NA WATU (Anti Social)
-----------------------------------
Nimekuwa nikiwaamini watu sana na kushirikiana kwa karibu na watu saana kwa kipindi cha nyuma, isipokuwa nikaja kutambua kuwa nilifanya makosa!
Sawa umetutolea dalili za Stress isipokuwa kwa mimi binafsi nimekuwa na mwenendo wa kujitakia wa (Anti Social) yaani (najikataa) sipendelei mwenyewe kukaa na watu saana kutokana na mambo yaliyonitokea hapo nyuma ya kuamini sana watu na kushirikiana na watu sana kwa karibu yamekuwa yakiniletea gharama zaidi kuliko faida.
Imetokea watu ninao shirikiana nao wanakuwa ndio mwanzo wa Kuhujumiwa na kukwama ktk shughuli zangu za kazi na maisha yangu kuanikwa kwa mambo nisivyo ridhia, hivyo nilifanya uchunguzi nikagundua kuwa waliohusika ni watu ninaoshirikiana nao, hivyo nikabadili mwenendo nikaamua kuwa sina Rafiki wa kudumu au kuwa karibu sana na watu.
Mbona kwa kutokuwa karibu na watu kama zamani naona sina tatizo lolote?
JE HII ITAKUWA NI DALILI YA STRESS?
kujichanganya na watu haimaanishi ukaanike mambo yako hadharani unaweza kukaa na kampani lakini ukajua tu mipaka yako sio kuwamwagia mchele wote ndio mwanzo wa kukudhuru, la msingi ukishawajua wabaya unajiepusha au unajua jinsi ya ku dili nao, kukaa mwenyewe sana napo si kuzuri unaweza ukachanganyikiwa
Mdau Anonyomus wa February 15, 2012 12:07 PM
Kujichanganya na watu,
Sawa tumeelewa msisitizo wako kuhusu kujichanganya na watu na kuwa na tahadhari kuwamwagia mchele Wabaya katika makundi yetu ya mikusanyiko.
TATIZO NI KUWA HATA KAMA UTAJARIBU KUFICHA SIRI ZAKO ZA NDANI PANA WATU NI WAFUATILIAJI SANA WA MAMBO YA WENZAO NA WAMBEA, SASA SI BORA KUJIKATAA KABISA ILI KUKWEPA HATARI YA KUFUATILIWA NA KUCHUNGUZWA HADI SIRI ZAKO ZITOKE?
Mtoa Maoni wa 8 hapo juu,
Duhhh bahati mbaya sana pana Methali isemayo 'Kikulacho ki nguoni mwako'
Watu hupenda kujitenga na makundi na kujichanganya na watu kwa kuogopa kufuatiliwa na kuchunguzwa mambo yao.
Ni vigumu sana kuwadhibiti Watu wanapo taka kukufuatilia ,tena inakuwa hatari zaidi kama watakufuatilia kwa nia mbaya ni lazima wakulaze chali watimize lengo halafu wakucheke!
1.Huwezi amini watu wanafuatilia hadi maongezi ya simu, utashangaa ukikaa na watu kila simu ikiingia au ukipiga wana sikiliza maongezi yako ki mtindo kama vile sio kumbe wanafuatilia!
2.Huwezi amini, unaweza ukawa unafahamiana na watu fulani, halafu masuala yako wanawauliza watu wengine badala ya kukuuliza wewe muhusika!
(Unashangaa mambo yako unayasikia kwa watu ambao hukuwapa taarifa hizo mwenyewe na unastaajabu kuona yamefika fika vipi kwao?)
MNAONA SASA AINA YA MARAFIKI WANAFIKI MAKUNDI 1 NA 2 HAPO JUU? HAWA WASHIRIKA WA NAMNA HII NDIO SABABU YA WATU KUAMUA KUWA ANTI SOCIAL (KUJITENGA NA KUTOKUJICHANGANYA NA WATU) ILI KUJINUSURU NA SUMU KALI YA UBAYA KUPITIA TIKETI YA KUFAHAMIANA NA KUWA KARIBU SANA KIJAMII:
Watu wameona waamue kujitenga kabisa na watu, lakini wanajichanganya ki usanii tu na watu lakini inakuwa KIMWILI WAPO NA WATU LAKINI KIROHO WAMEJITENGA MBALI NA WATU!
kutokwa n chunusi na kuwa na mabaka usoni coz mara nying unavyowaza unatumbua chunusi nyingne hata hazijatokeza kivile na kurudia kutumbua machunusi madonda ambayo ulishatumbua it has happen to me
Post a Comment